Muslim Library

Surah An-Naba' ( The Great News )

Swahili

Surah An-Naba' ( The Great News ) - Aya count 40
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ ( 1 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 1
WANAULIZANA nini?
عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ ( 2 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 2
Ile khabari kuu,
الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ ( 3 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 3
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ ( 4 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 4
La! Karibu watakuja jua.
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ ( 5 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 5
Tena la! Karibu watakuja jua.
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا ( 6 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 6
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا ( 7 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 7
Na milima kama vigingi?
وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا ( 8 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 8
Na tukakuumbeni kwa jozi?
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا ( 9 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 9
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا ( 10 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 10
Na tukaufanya usiku ni nguo?
وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا ( 11 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 11
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا ( 12 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 12
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا ( 13 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 13
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
وَأَنزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاءً ثَجَّاجًا ( 14 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 14
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
لِّنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا ( 15 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 15
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا ( 16 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 16
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا ( 17 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 17
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا ( 18 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 18
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
وَفُتِحَتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ أَبْوَابًا ( 19 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 19
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا ( 20 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 20
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا ( 21 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 21
Hakika Jahannamu inangojea!
لِّلطَّاغِينَ مَآبًا ( 22 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 22
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
لَّابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا ( 23 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 23
Wakae humo karne baada ya karne,
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا ( 24 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 24
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا ( 25 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 25
Ila maji yamoto sana na usaha,
جَزَاءً وِفَاقًا ( 26 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 26
Ndio jaza muwafaka.
إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا ( 27 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 27
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا ( 28 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 28
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا ( 29 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 29
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا ( 30 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 30
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا ( 31 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 31
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا ( 32 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 32
Mabustani na mizabibu,
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا ( 33 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 33
Na wake walio lingana nao,
وَكَأْسًا دِهَاقًا ( 34 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 34
Na bilauri zilizo jaa,
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا ( 35 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 35
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
جَزَاءً مِّن رَّبِّكَ عَطَاءً حِسَابًا ( 36 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 36
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
رَّبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا ( 37 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 37
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًا ( 38 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 38
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ مَآبًا ( 39 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 39
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
إِنَّا أَنذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا ( 40 ) An-Naba' ( The Great News ) - Aya 40
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah